Mkoa wa kigoma watia fora kwa idadi kubwa ya wakimbizi toka nchini Burundi. | nyula blog

Habari Kila Pande

Breaking News
Loading...

Wednesday, January 27, 2016

Mkoa wa kigoma watia fora kwa idadi kubwa ya wakimbizi toka nchini Burundi.


Idadi ya wakimbizi toka nchini Burundi wanaoingia nchini imezidi kuongezeka ambapo sasa ni wastani wa wakimbizi mia 200 hadi mia 300 hupokelewa kila siku na kusababisha serikali na mashirika yanayotoa huduma kwa wakimbizi kuzidiwa uwezo wa kutoa huduma na hasa huduma za afya.
Hali hiyo imeelezwa na katibu tawala wa mkoa wa Kigoma Mhandisi John Ndunguru wakati akipokea msaada wa vifaa vya kusaidia akinamama kujifungua kutoka shirika la World Lung Foundation ambapo amesema hali ya huduma za afya kwa wananchi na katika makambi ya wakimbizi si za kuridhisha kutokana na idadi kubwa ya mahitaji ikilinganishwa na wataalam na vifaa vilivyopo ambapo amesema hadi sasa mkoa una zaidi ya wakimbizi laki moja na elfu 70 katika makambi ya Nyarugusu na Nduta.
 
Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa shirika la World Lung Foundation nchini Dk.Nguge Mwakatundu amesema wameamua kutoa vifaa hivyo ili kusaidia kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi na kuepusha upasuaji usio wa lazima huku kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Kigoma Dk Fadhil Kibaya akieleza kuwa vituo tisa vya afya vitanufaika na msaada huo.
 
Download Video and Put Comment
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin